Picha ya jengo la taasisi
Bodi ya Korosho

Kuhusu Bodi ya Korosho Tanzania

Bodi ya Korosho Tanzania (CBT) ni chombo cha ushirika kilichoanzishwa kwa Sheria Sura ya 203 RE 2023. Imekabidhiwa jukumu la kusimamia maendeleo ya Sekta ya Korosho nchini Tanzania katika kutekeleza majukumu yake. Bodi ya Korosho inatilia mkazo zaidi katika kuboresha obora na ufanisi katika sekta ndogo ya korosho ili kukidhi matakwa ya wadau mbalimbali na hivyo kuwawezesha kuchangia katika maendeleo ya Taifa.

Dira Yetu

Kuwa taasisi ya udhibiti yenye uwezo na ufanisi kwa ajili ya sekta ya korosho iliyo hai na endelevu.

Dhima Yetu

Kukuza, kusimamia na kudhibiti masuala yote katika sekta ya korosho kwa ufanisi, kwa tija, na kwa haki.

Maadili ya Msingi

Uadilifu

Tunazingatia uwazi, ukweli na uaminifu katika utoaji wa huduma zetu zote kwa umma na wadau wa korosho.

Weledi

Tunatumia ujuzi, maarifa, na viwango vya juu vya kiutendaji katika kutekeleza majukumu yetu ya kila siku.

Ubunifu

Tunahamasisha matumizi ya teknolojia mpya na njia bora za kisasa kutatua changamoto za tasnia ya korosho.

Ushirikiano

Tunathamini mchango wa kila mdau na kufanya kazi kwa umoja ili kufikia malengo yetu ya pamoja.

Uwajibikaji

Tunawajibika kwa maamuzi na matendo yetu, tukihakikisha rasilimali zinatumika kwa ufanisi na tija kwa maendeleo ya kilimo.